Muuguzi anusuru watoto watatu kutoka hospitali iliyokumbwa na mlipuko mjini Beirut

Maelezo ya video, Muuguzi anusuru watoto waliokuwa kwenye hospitali iliyokumbwa na mlipuko mjini Beirut
Iliyochapishwa

Muuguzi alifanikiwa kunusuru watoto njiti waliokuwa tu ndio wamezaliwa katika hospitali hiyo baada kutokea kwa mlipuko mkubwa ulioharibu bandari ya Beirut. “Hatukuwa na mashine za kusaidia watoto kupumua na watoto hawangeweza kukaa kwa zaidi ya saa moja bila mashine hizo,” Pamela Zaynun ameiambia BBC. Juhuzi zake za kunusuru watoto hao na kuhakikisha wamefika eneo salama ni kitendo ambacho kimezungumziwa sana katika mitando ya kijamii.